Loading...

ZOUMA NJE MIEZI SITA

 Kurt Zouma


Beki wa klabu ya Chelsea, Mfaransa Kurt Zouma atakua nje ya uwanja kwa muda unaokadiriwa kufika miezi sita kufuatia jeraha la goti alilopata katika mechi ya weekend hii dhidi ya Manchester United.
Zouma aliumia goti lake wakati akigombea mpira na kiungo wa United Michael Carrick na madaktari wamethibitisha atalazimika kufanyiwa upasuaji.
Katika akaunti yake ya Twiter Zouma alithibitisha kuumia kwa goti lake na kwamba upasuaji utafanyika muda wowote hivi karibuni huku akiwashukuru watu wote ambao wamekua wakimtumia message za pole.
Kwa maana hiyo Mfaransa huyo atakosa michuano ya Ulaya ambayo itafanyikia nchini kwake hapo baadae June akiwa ameshacheza mechi mbili za timu ya Taifa toka aitwe kwa mara ya kwanza.
Wachezaji mbalimbali wameendelea kumtumia salamu za pole na kumtakia pone haraka huku wakiongozwa zaidi na wachezaji wa Ufaransa.
Kiungo wa United, Morgan Schneiderlin aliandika katika ukurasa wake wa Instagram "Pole sana kwa kuumia, natumaini utarudi tena ukiwa imara zaidi".
Zouma lijiunga na Chelsea akitokea klabu ya St Ettiene ya Ufaransa katika dirisha la mwaka 2014 na ametengeneza ukuta mzuri pamoja na mkongwe John Terry ambae amethibitisha kuiacha klabu hiyo baada ya msimu huu.

MOURINHO AFANYA MAZUNGUMZO NA MABOSS WA MANCHESTER UNITED

Jose Mourinho and Louis van Gaal 


Uongozi wa klabu ya Manchester United umefanya mazungumzo na wawakilishi wa Kocha aliyeachwa na Chelsea, Jose Mourinho.
Mourinho, 53 aliefukuzwa na Chelsea mwezi Desemba ana matumaini makubwa ya kupata kibarua hicho akimrithi Louis van Gaal ambaye amekua na wakati mgumu Old Trafford kufuatia kiwango hafifu cha timu hiyo kwa miezi ya karibuni.
Hakuna maelewano rasmi yaliyofikiwa baina ya pande hizo mbili na klabu haijatoa taarifa yoyote rasmi lakini kuna kila dalili akapata dili hilo huku ujio wa kocha Pep Giardiola ukiongeza hamasa ya Morinho kubakia England ili apambane na hasimu wake wa zamani akiwa Real Madrid.
Van Gaal anajiandaa kuiacha klabu hiyo baada ya msimu huu, ikiwa ni msimu mmoja tofauti na ilivyotarajiwa kama mkataba wake unavyosema.
Hii inatoa picha kuwa Mourinho ndiye mrithi pekee wa Van Gaal baada ya msimu huu. Mreno huyo hajafanya mazuzngumzo na klbau yoyote toka aachie ngazi Stamford Bridge na United haijawasiliana na kocha yeyote toka Manchester United iwe na matokeo mabovu ikiwemo kutolewa kwenye Michuano ya klabu bingwa Ulaya, UEFA.


That would leave the way clear for Mourinho, who is known to be excited by the prospect of taking over at Old Trafford.


WANAJESHI 120 WAUAWA NCHINI SYRIA

 Syrian woman fleeing embattled city of Aleppo in Bab al-Salam, next to the city of Azaz. 5 Feb 2016


Mapambano makali yameibuka jirani na mji wa Allepo kaskazini mwa Syria wakati majeshi ya Serikali yakijaribu kuwazunguka waasi waliojificha katika mahandaki.
Kundi la Wachunguzi wa Haki za Binadamu la Syria limesema wanajeshi zaidi ya 120 kutoka katika pandezote mbili wameuawa kwenye mji wa Ratyan Ijumaa hii.
Zaidi ya wakimbizi 20, 000 walikimbia mapigano yanayoendelea wakijaribu kuvuka mpaka wa Syria kuelekea nchini Uturuki.
Uturuki imesema imejiandaa kuwasaidia wakimbizi ingawa mipaka imefungwa. Siku chache zilizopita majeshi ya Syria yalisaidiwa msaada wa silaha za anga na majeshi ya Urusi katika mji wa Allepo.
Ijumaa hii televisheni ya Taifa ya nchini Syria ilisema majeshi ya waasi yaliuteka mji wa Ratyan ulioko kaskazini kidogo mwa mji wa Allepo.

STURRIDGE AUMIA MAZOEZINI, KUKAA NJE TENA KWA MUDA ZAIDI

 Daniel Sturridge
Huku akiwa amekaribia kupona majeraha yake ya awali, mshambuliaji mwingereza wa Liverpool Daniel Sturridge amejiumiza tena na hivyo kukosekana katika mechi ijayo ya Kombe la Ligi dhidi ya Stoke City.
Sturridge a,echeza mechi sita tu msimu huu huku akicheza 19 kwa msimu uliuopita kufuatia kuandamwa na majeraha ya mara kwa mara jambo linalomuumiza kichwa kocha mpya wa timu hiyo, Jurgen Klopp.
Klopp sasa amebakiwa na chaguo moja tu la straika, Christian Benteke kwa sababu Daniel Ings na Divock Origi pia wanasumbuliwa na majeraha.
Sturridge hajacheza tangu aumie dhidi ya Newcastle December 6 mwaka jana na baada ya ushindi wa siku ya Boxing Day dhidi ya Leicester City alitweet kuwa amerudi mazoezini na hali yake iko vizuri.

ZIDANE APEWA MIKOBA YA BENITEZ REAL MADRID

 Zinedine Zidane (left) and president Florentino Perez
Nguli wa soka ambaye alitengeneza jina akiwa katika Uwanja wa Santiago Bernabeu, Zinedine Zidane ameteuliwa rasmi kuiongoza klabu hiyo kufuatia kutimuliwa kwa Mhispania Rafael Benitez kufuatiua mwenendo mbovu wa timu hiyo toka achukue kiti hicho.
Benitez, 55 amekua na msimu mbovu na Real Madrid ikiwemo uhusiano wake na staa wa klabu hiyo Cristiano Ronaldo jambo lilioanza kuonyesha dalili mbaya za siku za Benitez klabuni hapo.
Benitez ametimuliwa baada ya kikao cha bodi kilichokaa jana Jumatatu na kuamua kumpa majukumu mchezaji huyo wa zamani wa Ufaransa na mshindi wa Kombe la Dunia la 1998.
Zidane, 43 ameonyesha kufurahia uteuzi huo huku akisema ni furaha ya pekee kufundisha klabu kubwa kama Real Madrid yenye historia ya pekee Ulaya.
Zidane ataanza kazi rasmi Jumamosi hii ambapo ataivaa Deportivo la Coruna jkatika dimba la Bernabeu huku akiwa ni kocha wa 11 kuteuliwa katika kipindi cha miaka 12 ya utawala wa Rais Florentino Perez klabuni hapo.
Benitez amepoteza michezo mitatu tu kati ya 25 huku akiipeleka Real katika hatua ya 16 bora kwenye Klabu Bingwa Ulaya. Ushindi wa 8-0 dhidi ya Malmo na ule wa 10-2 dhidi ya Rayo Valecano ni miongoni mwa mechi za kukumbukwa za kocha huyo akiwa Madrid. 
Kuondoka kwa Benitez kunaweza kuwa kumechangiwa na masuala kadhaa ikiwemo kipigo cha aibu kutoka kwa mahasimu wao wakuu Barcelona cha 4-0 pale Bernabeu jambo linalosemekana kuzua ugomvi katio yake na staa wa timu hiyo, Ronaldo. 
Zidane anapewa mikoba hiyo  huku Florentino akigoma kusema mkataba waliompa nguli hiyo aliyekua kwenye benchi la ufundi la Team B ya Real Madrid.

RATIBA YA LIGI KUU UINGEREZA WIKIENDI HII IKO HAPA

Sat 2 Jan 2016 - Premier League
  • West Ham v Liverpool 12:45
  • Arsenal v Newcastle 15:00
  • Leicester v Bournemouth 15:00
  • Man Utd v Swansea 15:00
  • Norwich v Southampton 15:00
  • Sunderland v Aston Villa 15:00
  • West Brom v Stoke 15:00
  • Watford v Man City 17:30
Sun 3 Jan 2016 - Premier League
  • Crystal Palace v Chelsea 13:30
  • Everton v Tottenham 16:00
Tue 12 Jan 2016 - Premier League
  • Aston Villa v Crystal Palace 19:45
  • Bournemouth v West Ham 19:45

KIPA SUNDERLAND ATOA MSAADA WA EURO 5,000 KWA VIZIWI.

 Jack Butland


Kipa wa Stoke City, Mwingereza Jack Butland ametoa Euro 5,000 kwa ajilim ya timu ya Taifa ya Wanawake  Uingereza ya Viziwi ili waweze kushiriki michuano ya Kombe la Dunia ya Viziwi nchini Italy June mwaka huu.
Butland aliandika kwenye ukurasa wake wa Twitter kuwa amejifunza mengi sana kutoka kwenye michuano mikubwa na amepata uzoefu mkubwa kwahyo alitaka kuwasaidia nao wapate uzoefu huo.
Pamoja naye, wachezaji wengine wa Kiingereza Lucy Bronze, Jade Moore, Jo Potter na Fran Kirby wamechangia ili kufanikisha jambo hilo huku kiwango kinachohitajika ni Euro 20, 000.
Butland, ambaye amecheza mechi tatu na England, pia ni balozi wa kampeni ya ubaguzi wa rangi ya Kick Out Discriminatio.

UNITED YAANDAA PAUNI 35mil KUMPATA ANDERSON

Man Utd set to offer Lazio £35m for Felipe Anderson 
Manchester United inajiandaa kutuma ofa ya pauni mil 35 kwa ajili ya kupata huduma ya mchezaji wa Lazio, Mbrazil Felipe Anderson ambaye anakipiga Lazio nchini Italia. United inatarajia kufanya uhamisho huo kuwa wa kwanza katika dirisgha dogo la usajili lililofunguliwa rasmi leo.
Anderson, 22 anasakwa na United ambayo inahaha baada ya kucheza michezo 8 bila ya ushindi jambo linalomlazimisha Ed Woodward kufanya kazi ya kumfatilia mbrazili huyo ili kuimarisha kikosi chake.
Hii si mara ya kwanza kwa United kumfukuzia mchezaji huyo, mara baada ya Van Gaal kupewa kazi Old Trafford alifanya juhudi kumnasa ikashindikana lakini kufuatia fomu mbaya ya kikosi hicho inawalazimu kumnunua Anderson.
Van Gaal na Ed Woodward walishuhudia timu hiyo ikitumia karibu Pauni 100 milioni katika kiangazi kilichopita lakini wako tayari kuvunja benki tena kufanya usajili kuimarisha safu ya ushambuliaji ambayo imehangaika kuliona lango msimu huu.
Mazungumzo baina ya timu hizo yameanza siku 10 zilizopita huku United wakiwa tayari kulipa milioni 25 kupata saini ya mchezaji huyo wa zamani wa Santos ambaye amecheza mechi yake ya kwanaza na Brazil June mwaka 2015.

Licha ya Anderson kukosa uzoefu wa timu ya Taifa lakini United ina imani kuwa mchezaji huyo atawafaa mabingwa hao mara 20 wa Ligi Kuu ya Uingereza.

 

VAN GAAL; NASTAAFU BAADA YA KAZI UNITED

Van Gaal: Manchester United job could be my last  

Kocha wa Manchester United, Louis Van Gaal amekiri kuwa baada ya kuifundisha timu hiyo atafikiria kustaafu rasmi kazi hiyo. Van Gaal amekana kuhusu uamuzi huo kuhusishwa na mwenendo wa klabu hiyo inayosua sua baada ya kucheza michezo nane bila ya ushindi wowowte katika michuano yote huku akiishuhudia timu hiyo ikishuka hadi nafasi ya sita kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya Uingereza.
 Droo iliyopatikana dhidi ya Chelsea wiki hii jumatatu ilipunguza presha kwa kocha huyo baada ya kupokea vipigo vitatu mfululizo kutoka kwa Bournermouth, Norwich City, Stoke City jambo lililozua shaka juu ya kibarua cha Mholanzi huyo aliyekua kocha wa Uholanzi katika michuano ya Kombe la Dunia iliyofanyika Brazili kiangazi cha 2014.
United itavaana na Swansea wikiendi hii huku Van Gaal akiwa na kumbukumbu mbaya dhidi ya kikosi hicho, ameshindwa kuifunga timu hiyo katika mechi zote tatu walizokutana akiambulia vipigo tu.
Jina la Jose Mourinho linatajwa sana kwenye midomo ya mashabiki wa timu hiyo jambo linaloonyesha kuchoshwa na falsafa ya Mholanzi huyo. Kwenye mechi dhidi ya Chelsea muuzaji wa bidhaa za Manchester Ubited nje ya uwanja wa Old Traford alionekana amebeba skafu zenye rangi nyekundu na jina la Mourinho jambo linaloonyesha mwisho wa Mholanzi huyo unakaribia huku bodi ya timu hiyo ikiendelea kumvumilia.


Newer Posts
© Copyright +255 ONLINE | Designed By AFROPIXELS MEDIA CO. LTD
Back To Top