▼▼▼TO SEE PHOTOS AND THE VIDEO CLICK HERE DOWN▼▼▼
Huku akiwa amekaribia kupona majeraha yake ya awali, mshambuliaji mwingereza wa Liverpool Daniel Sturridge amejiumiza tena na hivyo kukosekana katika mechi ijayo ya Kombe la Ligi dhidi ya Stoke City.
Sturridge a,echeza mechi sita tu msimu huu huku akicheza 19 kwa msimu uliuopita kufuatia kuandamwa na majeraha ya mara kwa mara jambo linalomuumiza kichwa kocha mpya wa timu hiyo, Jurgen Klopp.
Klopp sasa amebakiwa na chaguo moja tu la straika, Christian Benteke kwa sababu Daniel Ings na Divock Origi pia wanasumbuliwa na majeraha.
Sturridge hajacheza tangu aumie dhidi ya Newcastle December 6 mwaka jana na baada ya ushindi wa siku ya Boxing Day dhidi ya Leicester City alitweet kuwa amerudi mazoezini na hali yake iko vizuri.
TANGAZO LA NDANI===
Facebook Blogger Plugin by AFROPIXELS PLUGIN


Chapisha Maoni