▼▼▼TO SEE PHOTOS AND THE VIDEO CLICK HERE DOWN▼▼▼
Manchester United inajiandaa kutuma ofa ya pauni mil 35 kwa ajili ya kupata huduma ya mchezaji wa Lazio, Mbrazil Felipe Anderson ambaye anakipiga Lazio nchini Italia. United inatarajia kufanya uhamisho huo kuwa wa kwanza katika dirisgha dogo la usajili lililofunguliwa rasmi leo.
Anderson, 22 anasakwa na United ambayo inahaha baada ya kucheza michezo 8 bila ya ushindi jambo linalomlazimisha Ed Woodward kufanya kazi ya kumfatilia mbrazili huyo ili kuimarisha kikosi chake.
Hii si mara ya kwanza kwa United kumfukuzia mchezaji huyo, mara baada ya Van Gaal kupewa kazi Old Trafford alifanya juhudi kumnasa ikashindikana lakini kufuatia fomu mbaya ya kikosi hicho inawalazimu kumnunua Anderson.
Van Gaal na Ed Woodward walishuhudia timu hiyo ikitumia karibu Pauni 100 milioni katika kiangazi kilichopita lakini wako tayari kuvunja benki tena kufanya usajili kuimarisha safu ya ushambuliaji ambayo imehangaika kuliona lango msimu huu.
Mazungumzo baina ya timu hizo yameanza siku 10 zilizopita huku United wakiwa tayari kulipa milioni 25 kupata saini ya mchezaji huyo wa zamani wa Santos ambaye amecheza mechi yake ya kwanaza na Brazil June mwaka 2015.
Mazungumzo baina ya timu hizo yameanza siku 10 zilizopita huku United wakiwa tayari kulipa milioni 25 kupata saini ya mchezaji huyo wa zamani wa Santos ambaye amecheza mechi yake ya kwanaza na Brazil June mwaka 2015.
Licha ya Anderson kukosa uzoefu wa timu ya Taifa lakini United ina imani kuwa mchezaji huyo atawafaa mabingwa hao mara 20 wa Ligi Kuu ya Uingereza.
TANGAZO LA NDANI===
Facebook Blogger Plugin by AFROPIXELS PLUGIN


Chapisha Maoni