▼▼▼TO SEE PHOTOS AND THE VIDEO CLICK HERE DOWN▼▼▼
Kocha wa Manchester United, Louis Van Gaal amekiri kuwa baada ya kuifundisha timu hiyo atafikiria kustaafu rasmi kazi hiyo. Van Gaal amekana kuhusu uamuzi huo kuhusishwa na mwenendo wa klabu hiyo inayosua sua baada ya kucheza michezo nane bila ya ushindi wowowte katika michuano yote huku akiishuhudia timu hiyo ikishuka hadi nafasi ya sita kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya Uingereza.
Droo iliyopatikana dhidi ya Chelsea wiki hii jumatatu ilipunguza presha kwa kocha huyo baada ya kupokea vipigo vitatu mfululizo kutoka kwa Bournermouth, Norwich City, Stoke City jambo lililozua shaka juu ya kibarua cha Mholanzi huyo aliyekua kocha wa Uholanzi katika michuano ya Kombe la Dunia iliyofanyika Brazili kiangazi cha 2014.
United itavaana na Swansea wikiendi hii huku Van Gaal akiwa na kumbukumbu mbaya dhidi ya kikosi hicho, ameshindwa kuifunga timu hiyo katika mechi zote tatu walizokutana akiambulia vipigo tu.
Jina la Jose Mourinho linatajwa sana kwenye midomo ya mashabiki wa timu hiyo jambo linaloonyesha kuchoshwa na falsafa ya Mholanzi huyo. Kwenye mechi dhidi ya Chelsea muuzaji wa bidhaa za Manchester Ubited nje ya uwanja wa Old Traford alionekana amebeba skafu zenye rangi nyekundu na jina la Mourinho jambo linaloonyesha mwisho wa Mholanzi huyo unakaribia huku bodi ya timu hiyo ikiendelea kumvumilia.
United itavaana na Swansea wikiendi hii huku Van Gaal akiwa na kumbukumbu mbaya dhidi ya kikosi hicho, ameshindwa kuifunga timu hiyo katika mechi zote tatu walizokutana akiambulia vipigo tu.
Jina la Jose Mourinho linatajwa sana kwenye midomo ya mashabiki wa timu hiyo jambo linaloonyesha kuchoshwa na falsafa ya Mholanzi huyo. Kwenye mechi dhidi ya Chelsea muuzaji wa bidhaa za Manchester Ubited nje ya uwanja wa Old Traford alionekana amebeba skafu zenye rangi nyekundu na jina la Mourinho jambo linaloonyesha mwisho wa Mholanzi huyo unakaribia huku bodi ya timu hiyo ikiendelea kumvumilia.
TANGAZO LA NDANI===
Facebook Blogger Plugin by AFROPIXELS PLUGIN

Chapisha Maoni