Loading...

ZIDANE APEWA MIKOBA YA BENITEZ REAL MADRID

▼▼▼TO SEE PHOTOS AND THE VIDEO CLICK HERE DOWN▼▼▼
 Zinedine Zidane (left) and president Florentino Perez
Nguli wa soka ambaye alitengeneza jina akiwa katika Uwanja wa Santiago Bernabeu, Zinedine Zidane ameteuliwa rasmi kuiongoza klabu hiyo kufuatia kutimuliwa kwa Mhispania Rafael Benitez kufuatiua mwenendo mbovu wa timu hiyo toka achukue kiti hicho.
Benitez, 55 amekua na msimu mbovu na Real Madrid ikiwemo uhusiano wake na staa wa klabu hiyo Cristiano Ronaldo jambo lilioanza kuonyesha dalili mbaya za siku za Benitez klabuni hapo.
Benitez ametimuliwa baada ya kikao cha bodi kilichokaa jana Jumatatu na kuamua kumpa majukumu mchezaji huyo wa zamani wa Ufaransa na mshindi wa Kombe la Dunia la 1998.
Zidane, 43 ameonyesha kufurahia uteuzi huo huku akisema ni furaha ya pekee kufundisha klabu kubwa kama Real Madrid yenye historia ya pekee Ulaya.
Zidane ataanza kazi rasmi Jumamosi hii ambapo ataivaa Deportivo la Coruna jkatika dimba la Bernabeu huku akiwa ni kocha wa 11 kuteuliwa katika kipindi cha miaka 12 ya utawala wa Rais Florentino Perez klabuni hapo.
Benitez amepoteza michezo mitatu tu kati ya 25 huku akiipeleka Real katika hatua ya 16 bora kwenye Klabu Bingwa Ulaya. Ushindi wa 8-0 dhidi ya Malmo na ule wa 10-2 dhidi ya Rayo Valecano ni miongoni mwa mechi za kukumbukwa za kocha huyo akiwa Madrid. 
Kuondoka kwa Benitez kunaweza kuwa kumechangiwa na masuala kadhaa ikiwemo kipigo cha aibu kutoka kwa mahasimu wao wakuu Barcelona cha 4-0 pale Bernabeu jambo linalosemekana kuzua ugomvi katio yake na staa wa timu hiyo, Ronaldo. 
Zidane anapewa mikoba hiyo  huku Florentino akigoma kusema mkataba waliompa nguli hiyo aliyekua kwenye benchi la ufundi la Team B ya Real Madrid.

TANGAZO LA NDANI===
Facebook Blogger Plugin by AFROPIXELS PLUGIN

Chapisha Maoni

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright +255 ONLINE | Designed By AFROPIXELS MEDIA CO. LTD
Back To Top