Loading...

WANAJESHI 120 WAUAWA NCHINI SYRIA

▼▼▼TO SEE PHOTOS AND THE VIDEO CLICK HERE DOWN▼▼▼
 Syrian woman fleeing embattled city of Aleppo in Bab al-Salam, next to the city of Azaz. 5 Feb 2016


Mapambano makali yameibuka jirani na mji wa Allepo kaskazini mwa Syria wakati majeshi ya Serikali yakijaribu kuwazunguka waasi waliojificha katika mahandaki.
Kundi la Wachunguzi wa Haki za Binadamu la Syria limesema wanajeshi zaidi ya 120 kutoka katika pandezote mbili wameuawa kwenye mji wa Ratyan Ijumaa hii.
Zaidi ya wakimbizi 20, 000 walikimbia mapigano yanayoendelea wakijaribu kuvuka mpaka wa Syria kuelekea nchini Uturuki.
Uturuki imesema imejiandaa kuwasaidia wakimbizi ingawa mipaka imefungwa. Siku chache zilizopita majeshi ya Syria yalisaidiwa msaada wa silaha za anga na majeshi ya Urusi katika mji wa Allepo.
Ijumaa hii televisheni ya Taifa ya nchini Syria ilisema majeshi ya waasi yaliuteka mji wa Ratyan ulioko kaskazini kidogo mwa mji wa Allepo.
TANGAZO LA NDANI===
Facebook Blogger Plugin by AFROPIXELS PLUGIN

Chapisha Maoni

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright +255 ONLINE | Designed By AFROPIXELS MEDIA CO. LTD
Back To Top